Mungu Kaniita
| Mungu Kaniita | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Album | MSHIPI (VOL. 22) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | F. Mtegeta | 
| Views | 8,603 | 
Mungu Kaniita Lyrics
- Tazama Mungu kaniita kati yao wanyonge
 nimtumikie yeye
 Tazama amenichagua kati ya viumbe
 nimuimbie yeye
 {Nitashangilia, sitaona haya,
 nitaruka kama ndama a haa
 Nami nitayatangaza bila woga
 matendo yake kwa mataifa } *2
- Mungu amenichagua, mimi amenichagua
 Tena akanitakasa na kunibariki, nimuimbie
- Furaha yangu kubwa, hii ni kuimba Nimwimbie
 Mungu wangu nyakati hizi za ujana ujana wangu
- Tujalie ujasiri, uvumilivu, wa kutangaza
 Neno lako Mungu kwao mataifa, wakufuate.
- Natarajia ushindi, siku ya mwisho, Nishangilie
 Na nifurahiye utukufu wako, milele yote
 
  
         
                            