Mwili wa Bwana Yesu
Mwili wa Bwana Yesu | |
---|---|
Choir | Sauti Tamu Melodies |
Album | Zilipendwa |
Category | Ekaristia (Eucharist) |
Composer | F. A. Nyundo |
Source | Tanzania |
Video | Watch on YouTube |
Musical Notes | |
Time Signature | 3 8 |
Music Key | A |
Notes | Open PDF |
Mwili wa Bwana Yesu Lyrics
-
Mwili wa Bwana Yesu, chakula cha mbingu
Ni chakula cha roho, chenye uzima
Hima uwe nasi ee Bwana Yesu
Ukatushibishe chakula bora
Ni chakula cha roho, chenye uzima -
Yesu alituambia, Yeye ni chakula
Ni chakula cha roho, chenye uzima
Anilaye mimi na kunywa damu
Anao uzima wa siku zote
Ni chakula cha roho, chenye uzima -
Yesu alituambia, kuwa tumpokee
Ni chakula cha roho, chenye uzima
Sote twaamini, ni mwili wake
Pia twaamini ni damu yake
Ni chakula cha roho, chenye uzima -
Hii ndiyo karamu, aliyotuachia
Ni chakula cha roho, chenye uzima
Ee Bwana Mwokozi tunakuomba
Kwa chakula hiki tuimarike
Ni chakula cha roho, chenye uzima