Mwimbieni Bwana
   
    
     
         
          
            Mwimbieni Bwana Lyrics
 
             
            
- Mwimbieni Bwana, mataifa ya dunia
 Mwimbieni Bwana litukuzeni jina lake
- Tangazeni wokovu wake siku kwa siku
 Yaelezeni mataifa utukufu wake
- Utukufu na uzuri unamtangulia, Enzi na
 wangavu zimo katika kikao chake kitakatifu
- Mpeni Bwana enyi jamii za mataifa
 Mpeni Bwana sifa na enzi
- Mpeni Bwana utukufu wa jina lake
 Toeni sadaka ingieni katika sebule zake
- Semeni kati ya mataifa, Bwana ni mfalme
- Atatawala ulimwengu kwa haki
 Na mataifa kwa uaminifu wake
- Atukuzwe Baba na mwana, na Roho Mtakatifu
 kama mwanzo na sasa, na siku zote milele.
 Amina.