Na Ahimidiwe Bwana
| Na Ahimidiwe Bwana | |
|---|---|
| Alt Title | Enyi Watumishi wa Bwana |
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha |
| Album | Nikiziangalia Mbingu (vol 18) |
| Category | Entrance / Mwanzo |
| Composer | P. F. Mwarabu |
| Views | 7,692 |
Na Ahimidiwe Bwana Lyrics
Enyi watumishi wa Bwana sifuni
Lisifuni lisifuni Jina la Bwana
Na ahimidiwe Bwana Mungu
Bwana Mungu kutoka Sayuni
Akaaye Yerusalemu aleluya
Na ahimidiwe Bwana Mungu
Bwana Mungu kutoka Sayuni
Akaaye Yerusalemu aleluya- Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana
Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu
Msifuni Bwana kwa kuwa yu mwema
Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza - Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo
Na Israeli wawe watu wake hasa
Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu
Na Mungu wetu yu juu ya miungu yote - Enyi mlango wa Israeli mhimidini
Enyi mlango wa Haruni mhimidini
Enyi mlango wa Lawi himidini Bwana
Enyi mnaomcha Bwana mhimidini Bwana