Na Ahimidiwe Bwana
| Na Ahimidiwe Bwana | |
|---|---|
| Alt Title | Enyi Watumishi wa Bwana | 
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Album | Nikiziangalia Mbingu (vol 18) | 
| Category | Entrance / Mwanzo | 
| Composer | P. F. Mwarabu | 
| Views | 7,301 | 
Na Ahimidiwe Bwana Lyrics
- Enyi watumishi wa Bwana sifuni
 Lisifuni lisifuni Jina la Bwana
 Na ahimidiwe Bwana Mungu
 Bwana Mungu kutoka Sayuni
 Akaaye Yerusalemu aleluya
- Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana
 Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu
 Msifuni Bwana kwa kuwa yu mwema
 Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza
- Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo
 Na Israeli wawe watu wake hasa
 Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu
 Na Mungu wetu yu juu ya miungu yote
- Enyi mlango wa Israeli mhimidini
 Enyi mlango wa Haruni mhimidini
 Enyi mlango wa Lawi himidini Bwana
 Enyi mnaomcha Bwana mhimidini Bwana
 
  
         
                            