Nani Kama Mama

Nani Kama Mama
Performed byOur Lady(Star of the Sea) Kenya Navy
AlbumTumeandamana
CategoryBikira Maria
ComposerAlfred Ossonga
Views6,557

Nani Kama Mama Lyrics

  1. Kwa ujasiri kwa sauti kubwa,
    nazitangaza sifa za mama [Maria]
    Nawauliza wakubwa wadogo,
    Ni nani kama mama [Maria]

    Alimzaaa Mungu mwenyewe [kweli]
    amewakomboa wana wa Eva [wote]
    Mama Maria anatuombea kwenye safari
    tufike salama [Mama Maria]
    Atungojea kule kwa mwanaye
    atupokee tuishi salama *2

  2. Kwa sifo tele kwa shangwe nderemo,
    Tujitokeze mbele za mama [Maria]
    Tucheze ngoma tupige makofi,
    vigelegele heko kwa mama [Maria]
  3. Salamu Mama umebarikiwa,
    Na baraka kuliko wote [Maria]
    Mzao wako amebarikiwa,
    Yesu mwanao ni Mungu kweli [Maria]
  4. Tukimbilie ulinzi wa mama,
    Tufunuliwe siri za Mbingu[Maria]
    Tupate shibe tupate neema,
    Tuwe na heri hata milele [Maria]