Nasimulia Sifa

Nasimulia Sifa
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumMbinguni Kutakuwa Raha (Vol 4)
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerJ. C. Shomaly
Views4,664

Nasimulia Sifa Lyrics

  1. { Nasimulia sifa za Bwana Mungu, tena na maajabu
    kwa viumbe wa duniani Mungu ni mtawala } *2

    Nashangaa lo! nashangaa lo! *2
    { Viwete wamepona, viziwi wamesikia,
    Bubu wamesemasema Mungu ni mtawala,
    kazi yake hutenda kwa haki } *2

  2. Kakusanya maji chungu chungu, maji ya bahari,
    Karatibisha udongo wenye rutuba
  3. Mwanga pia giza, kazitoa kwa ratiba yake,
    Mchana wa jua, usiku wa mbalamwezi
  4. Miti ya matunda, mingine isiyo na matunda,
    Mingine mirefu, mingine mifupi sana
  5. Enyi watu wote mwimbieni mwimbieni Mungu
    Lisifuni jina lake Mungu wa miungu.