Natamani Uwe Wangu
   
    
     
         
          
            Natamani Uwe Wangu Lyrics
 
             
            
- Nimekupenda nimevutiwa na wewe sikia-
 Ninatamani niwe wako uwe wangu siku zote
 Ndiwe chaguo la moyo wangu kwenye hii dunia-
 Ninatamani niwe wako uwe wangu siku zote
 Nitakusifu bila aibu hadharani (wewe)
 Nyimbo za shangwe hazitakauka kinywani
 (mwangu) Ingia mwangu,
 Yesu wangu kaa nami siku zote
- Nimewaona rafiki wengi wanaonivizia-
 Lakini wewe ndiye rafiki wa kweli na huria-
- Ulinipenda hata kabla mimi sijakusikia-
 Msalabani bila hatia Yesu ukanifia-
- Katika raha usikawie njoo kufurahia--
 Na kwenye shida sitachelewa nitakukimbilia--
- Nitakusifu milele yote nitakuhimidia--
 Nitaziimba fadhili zako nitazisimulia--