Navumilia Tu
| Navumilia Tu | |
|---|---|
| Performed by | Blessed Joseph Allamano Mshindo Iringa | 
| Album | Watu Wamekengeuka | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | F. F. Ngwila | 
| Views | 26,421 | 
Navumilia Tu Lyrics
- [s/a] Ninatazama juu angani nikiomba msaada
 Mateso yananizidi, hakuna anayekuja
 Nafungua mikono yangu naleta sala yangu
 Ee Bwana nisaidie, Mungu unihurumie
 Navumilia tu mimi ninavumilia tu
 (Bwana nateseka)/s/
 Navumilia tu, mimi ninavumilia tu,
 Navumilia tu, kwani haya yote yana mwisho
 Navumilia tu, mimi ninavumilia tu,
 Navumilia tu, kwani ipo siku yatakwisha
 /a2/
 Navumilia tu, ninavumilia tu mimi
 Navumilia tu, kwani haya yote yana mwisho
 Navumilia tu, ninavumilia tu mimi
 Navumilia tu, kwani ipo siku yatakwisha
 / t2 / a1 /
 Bwana nateseka, unihurumie kwa uwezo wako
 Naamini Bwana
 Nipo kwenye shida, Bwana niokoe sikati tamaa,
 Naamini Bwana, ipo siku yatakwisha
 /t/
 Navumilia tu mimi, ninavumilia tu
 Navumilia tu, kwani haya yote yana mwisho
 Navumilia tu mimi, ninavumilia tu
 Navumilia tu, kwani ipo siku yatakwisha
 /b/
 Navumilia tu mimi, navumilia tu mimi
 Navumilia tu, haya yote yana mwisho
 Navumilia tu mimi, navumilia tu mimi
 Navumilia tu, ipo siku yatakwisha
- Nalia kwa uchungu, machozi yananitiririka,
 Mateso ya dunia hii, naona yamekidhiri,
 Huyu mwovu shetani hakika ananisonga sana
 Ninakuomba ee Bwana unisaidie hima
 Navumilia tu mimi ninavumilia tu
 (Bwana nateseka)
- Vitisho vya dunia, magonjwa dharau masengenyo
 Na kunyanyasa wadogo, haya yote yatapita
 Nangojea kwa hamu, Bwana utakapokuja tena
 Nije niungane nawe, kwenye raha ya milele
 Navumilia tu mimi ninavumilia tu
 (Bwana nateseka)
- Ewe mama Maria, naomba uniombee mama
 Kwa Yesu mwanao mpenzi, ili aje aniokoe
 Roho mtakatifu Mungu anipe ujasiri,
 Hekima na pia nguvu, elimu pia uchaji
 Navumilia tu mimi ninavumilia tu
 (Bwana nateseka)
*Kwa wote walio katika taabu, uchungu na mateso ya aina yoyote; hasa WAGONJWA -
''Usikate tamaa, Mungu atasikia sala yako na atakufanyia miujiza. Ipo siku yatakwisha.''
  
 
 
 
  
         
                            