Mungu Yulee
   
    
     
         
          
            Mungu Yulee Lyrics
 
             
            
- { Nimemuona yule ninayemtafuta na neema zake
 Nimemuona -leo nimemuona Mungu } *2
 
 Mkononi mwake ana uzima tena ni wa milele
 Mkononi mwake ana uzima ninaoutafuta
 Na uzima huo anatoa bure kwa walio tayari
 Lakini kuna kanuni moja ya kwamba, uwajali watu.
- Nimemuona Mungu yu mtupu-u hana nguo
 Anatamani mimi niende nikamvishe
 Nimemuona Mungu ana njaa hana chakula
 Anatamani mimi niende nikamlishe
 Nimemuona Mungu ni mgonjwa-a kitandani
 Anatamani mimi niende kumtazama
- Nimemuona Mungu amefungwa-a gerezani
 Anatamani mimi niende kumfariji
 Nimemuona Mungu ni mkimbizi mpakani
 Anatamani mimi niende kumpokea
 Nimemuona Mungu ni yatima hana wazazi
 Anatamani mimi niende nikamtunze
- Nimemuona Mungu ni mjane hana matunzo
 Anatamani mimi niende kumhifadhi
 Nimemuona Mungu amefiwa ana majonzi
 Anatamani mimi niende kumfariji
 Nimemuona Mungu ni kilema na hajiwezi
 Anatamani mimi niende kumuinua
- Nimemuona Mungu atolewa angali mimba
 Anatamani mimi niende kumtetea
 Nimemuona Mungu anapigwa kwa makombora
 Anatamani mimi niende kusuluhisha
 Nimemuona Mungu ni mtumwa ananyanyaswa
 Anatamani mimi niende kumtetea