Nimeteuliwa na Mungu

Nimeteuliwa na Mungu
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumNimeteuliwa
CategoryUtume wa Uimbaji
ComposerAlfred Ossonga
Views8,767

Nimeteuliwa na Mungu Lyrics

  1. Nimeteuliwa na Mungu Baba nihubiri kwa kuimba*2
    { Nyimbo zinafundisha, nyimbo zaburudisha,
    Nyimbo zinafariji, roho zilizovunjika } *2

  2. Kila niamkapo nitamwimbia Bwana Mungu wangu
    Nitaimba nyimbo za kumtukuza aliyeniumba
  3. Mungu Baba Mwenyezi kaniteua mimi nihubiri
    Nihubiri kwa nyimbo nyimbo za shangwe nyimbo za Mbinguni
  4. Nafundisha kwa nyimbo naburudisha na ninafariji
    Natangaza ufalme wa Mungu Baba kwa njia ya nyimbo
  5. Sifa za Mungu Baba zimo kinywani mwangu siku zote
    Mimi nitaziimba sifa za Mungu daima milele