Ninafikiria Sana
| Ninafikiria Sana | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Mbinguni Kutakuwa Raha (Vol 4) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 6,233 | 
Ninafikiria Sana Lyrics
- Ninafikiria sana na kutafakari jambo hili mimi
 Jinsi ulimwengu ulivyogeukageuka kama kinyonga
 Ukweli umegeuka na kufanyika kuwa uwongo leo
 Msema kweli muovu muongo, yeye wakili wa mambo yote
 Shetani mbaya amezizunguka roho za watu
 Anawadanganya kwa mambo mazuri pia na anasa,
 Kanuni zake ngumu amri zake
 nazo zinashangaza shangaza
 Mbuzi wa kijani, ng`ombe wa dhambarau
 Kuku mwenye pembe, huyo utampata wapi
 Njoo kwake Yesu (Mwokozi) hahitaji haya (yote)
 Kanuni tubu dhambi, uingie mbinguni kwa baba
- Anakudanganya atakupa fedha uwe ni tajiri
 Kanuni zake yeye hudhulumu maskini na wajane
 Amelaaniwa amelaaniwa afanyaye haya,
 Kizazi chake yeye kitakuwa ni laana na fedheha
 Maisha yake yeye ni nchi kame na yenye chumvi nyingi
- Anakudanganya pombe inaweza kukuliwaza
 Utafune mifupa ungali bado ukiwa na meno
 Unafanya haya na watoto wako wanalala njaa,
 Na wewe kijana wazazi nyumba inawangukia
 Mwisho unapotea maisha yako wewe unachemsha
- Sikieni sasa enyi mnaoufanya ukahaba
 Mkijidanganya miili ni yenu sio ya yeyote
 Nani anaweza kujiongeza hata unywele wake
 Aliyekulea angefanya hivyo ungekuwa wapi
 Na Mungu naye asingekuumba wewe ungekuwa wapi
- Sikieni enyi mfanyao vita pia migogoro
 Hamuoni kuwa hayo ni machukizo kwake Mwenyezi,
 Mungu ameumba nchi nzuri yenye rutuba na mwanga
 Na sisi binadamu twaharibu kwa mabomu na risasi
 Tukumbuke ya kwamba mwisho tutalipa tutalipa haya
- Jukumu ni letu sasa tuzitubu dhambi zetu zote
 Tuliyoyafanya tumuombe Mola wetu asamehe,
 Tutakuwa safi dunia yote itajaa amani,
 Maisha yatakuwa ni rahisi utovu hamna tena,
 Na wote tutakuwa jamii yenye maendeleo bora
 
  
         
                            