Ninazo sababu
| Ninazo sababu | |
|---|---|
| Performed by | St. Francis of Assisi Kariobangi | 
| Album | Paazeni Sauti | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | Alfred Ossonga | 
| Views | 5,457 | 
Ninazo sababu Lyrics
- Ninazo sababu za kutoa shukrani zangu
 Ninakushukuru Bwana kwa ukarimu wako
 Ee Baba asante [sana] kwa upendo wako
 Pokea zawadi [hii], ninakutolea
 Â
- Enyi watu wa Mungu, njooni kwa masifu
 Kusanyikeni leo, mbele zake Bwana
 [Piga] pi- kelele, [piga] piga ngoma
 [Shangwe] sha- deremo, [piga] piga ‘kofi
 Â
- Mbingu pia dunia, ni mali ya Bwana
 Mito pia bahari, ni mali ya Bwana
 [Tuna]tu- sababu, [za ku]za- shukuru
 [Bwana]bwa- pokea, [shukra]shu- ni zetu
 Â
- Uhai wangu mimi, ni mali ya Bwana
 Sauti yangu nzuri, Bwana amenipa
 [Bwana] bwa- asante, [kwa we] kwa- ‘ma  wako
 [Naku] na- kwimbia, [naku] kuinua
 Â
- Natembea mchana, Bwana aniongoza
 Ninalala usiku, Bwana hunilinda
 [Bwana] bwa- asante, [kwa we] kwa- ‘ma  wako
 [Naku] na- shukuru, [naku] kutukuza
 
  
         
                            