Ningekuwa na Mabawa
Ningekuwa na Mabawa | |
---|---|
Choir | St. Joseph Migori |
Album | Mabawa |
Category | Entrance / Mwanzo |
Composer | Alfred Ossonga |
Ningekuwa na Mabawa Lyrics
Ningekuwa na mabawa, ningeruka hadi mbinguni
Ningekuwa na ufunguo, ningefungua mlango wako
{ Niingie nyumbani mwako, nikuimbie Mungu wangu
Katika makao yako, makao ya milele } *2
1. Malaika wanakuimbia nyimbo nzuri za furaha.
Makerubi hata maserafi wanasifu jina lako
2. Ningekuwa mimi ni bahari ningevuma kwa sauti
Ningekuwa mimi ni kengele ningelia usikie
3. Bwana mimi nitakuimbia siku za maisha yangu
Nitaimba sifa zako Bwana ili watu wasikie
4. Naamini kwamba siku moja nitafika mbele zako
Natamani sana kuja kwako kwenye raha ya milele
Favorite Catholic Skiza Tunes
SMS the Skiza ID to 811 to get the song as your Skiza tune.
Title | SKIZA ID |
Cha Kutumaini Sina | 5814855 |
Roho Yangu na Ikuimbie | 5814859 |
Nikupe Nini Mungu Wangu | 7482438 |
Sasa Wakati Umefika | 7482439 |
Nitakwenda Mimi Mwenyewe | 7482440 |
Zaeni Matunda Mema | 5814860 |
Bwana Kama Wewe Ungehesabu Maovu Yetu | 7482444 |
Huniongoza Mwokozi | 5814856 |
Utukuzwe Ewe Baba | 7482441 |
Tazama Tazama | 7482442 |