Ningelikuwa Kengele
| Ningelikuwa Kengele | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Habari Tuliyoleta (Vol 6) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 4,677 | 
Ningelikuwa Kengele Lyrics
- Ningelikuwa ni kengele mimi ningelia usikie!
 Ningelikuwa ni maua mimi ningechanua chanua
 Ili niupambe uso wako ewe Mungu uliyeniumba
 (Tena mimi) ukanipatia akili na mali ili nikutumikie
 { Naona fahari ninapotamka maneno haya,
 Ninapotazama kwa jinsi ulivyonipenda mimi kupita upeo } *2
- Umetamalaki Mungu (Mungu wangu),
 Nikulipe nini Bwana (hakika)
 Kila ninapotazama, wanadamu tulivyoumbika
- Akili na maarifa (yote hayo)
 Umetupatia Mungu (tazama)
 Sisi viumbe pekee, utashi nao ukatujaza
- Neema zako ni kuu (sana sana)
 Kwa wanao wote Baba (hakika),
 Mvua yako wainyesha hata kwa viumbe wenye dhambi
- Shukurani ninatoa (mimi Bwana),
 Kiumbe mnyonge Baba (naomba),
 Wabariki mayatima, na wale wasio na uwezo
 
  
         
                            