Nitasema
| Nitasema | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) |
| Album | Mshike Mshike (Vol 5) |
| Category | Thanksgiving / Shukrani |
| Composer | Marcus Mtinga |
| Views | 7,061 |
Nitasema Lyrics
{ Nitasema, nitasema mimi, nitasema, Mwenyezi Mungu
Kumbe ndiwe furaha moyoni mwangu } *2
{ Kwa heshima nitakutukuza Mungu wangu,
Tena kwa ujasiri, nitasimulia matendo yako siku zote } *2- Umeniona ukanihurumia,
Na kwa upole ukanisaidia,
Na kwa thamani sana nami naapa,
Sitaacha kukusifu milele - Ee Bwana mimi ni kitu gani kwako,
Unitazame hata unikumbuke,
Nina furaha matumaini makubwa,
Maana wanijali, sikia - Ee Mungu wangu wewe ni nguvu yangu,
Mimi muovu nakiri unyonge wangu,
Ni nani tena aliye kama wewe,
Na tena wanijali, tazama