Nitasema
| Nitasema | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Mshike Mshike (Vol 5) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | Marcus Mtinga | 
| Views | 6,946 | 
Nitasema Lyrics
- { Nitasema, nitasema mimi, nitasema, Mwenyezi Mungu
 Kumbe ndiwe furaha moyoni mwangu } *2
 { Kwa heshima nitakutukuza Mungu wangu,
 Tena kwa ujasiri, nitasimulia matendo yako siku zote } *2
- Umeniona ukanihurumia,
 Na kwa upole ukanisaidia,
 Na kwa thamani sana nami naapa,
 Sitaacha kukusifu milele
- Ee Bwana mimi ni kitu gani kwako,
 Unitazame hata unikumbuke,
 Nina furaha matumaini makubwa,
 Maana wanijali, sikia
- Ee Mungu wangu wewe ni nguvu yangu,
 Mimi muovu nakiri unyonge wangu,
 Ni nani tena aliye kama wewe,
 Na tena wanijali, tazama
 
  
         
                            