Saa ya Hukumu

Saa ya Hukumu
Performed byMaria Mt Mama wa Mungu Musoma
AlbumNchi Imejaa
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
ComposerMarcus Mtinga
Views8,169

Saa ya Hukumu Lyrics

  1. Saa ya hukumu yangu imefika,
    Na wakati wa kufa kwangu umekaribia
    Na kitabu cha kumbukumbu yangu kuwa wazi
    Yatakaposomwa matendo niliyotenda
    Katika siku za uhai wangu duniani
    Ni shimo lenye moto ajabu liko mbele yangu
    Ninajua nikitupwa humo uhai kwa heri
    Nitakwenda wapi mbona simba wamenizunguka
    Ninaangamia Bwana ona ninatapatapa.
    Sina msaada Bwana njoo unisaidie

  2. Ona adui zangu, sasa wanashangilia
    Hata rafiki zangu pia wamejiunga nao
    Wanasubiri kwa hamu waone hukumu yangu
    Hata mimi mwenyewe mapigo yananienda mbio
    Ninakuungamia Mungu wangu nisamehe makosa yangu
    Na ndugu zangu ninaomba radhi nimekosa nimekosa sana
  3. Moto unatisha, ni hatari kila upande
    Mwanga umepotea, giza limeshika hatamu
    Wanyama wenye njaa ona wanavyofurahia
    Na nyoka wenye sumu wanajiandaa kunidaka
    Na mimi najua bila wewe nimekwisha Mwokozi wangu
    Ee Mungu ninakulilia sikiliza ninavyolalamika
  4. Inuka ee Bwana, ili wote washangae
    Nyoosha mkono wako, niokoe ee Mungu wangu
    Kwa nguvu zako njoo, ee Bwana sema nitainuka
    Hata adui zangu washuhudie huruma yako
    Nishike mkono Mungu wangu niokoe naangamia
    Ee Bwana mapenzi yako yatimizwe nami nitashukuru
Also recorded by St. Cecilia choir, Zimmerman, Nairobi