Sitawaacha Kama Yatima

Sitawaacha Kama Yatima
ChoirSt. Mary's Kwa Njenga
AlbumSitawaacha Mayatima
CategoryRoho Mtakatifu (Pentecoste)

Sitawaacha Kama Yatima Lyrics

  1. Sitawaacha ninyi kama yatima,
    Sitawaacha ninyi (acha ninyi)
    Asema Bwana ( ee Bwana)
    Naja kwenu mioyo yenu ijae,
    Furaha na amani, asema Bwana
    Naja kwenu mioyo yenu ijae,
    Furaha na amani, asema Bwana
    eeh

  2. Nitawaombea ninyi kwa Baba yangu
    Naye atamtuma -Roho- wa kweli
    Huyo Roho Baba atakayemtuma
    Ndiye atakayewafariji mio-yo-ni
  3. Utukufu ulionipa ee Baba
    Nimewapa na wao -ili- wapate
    Kujua ndiwe peke uliyenituma
    Ukawapenda wao ulivyo-ni-pe-nda
  4. Baba hao ulionipa nataka
    Wawe pamoja nami, -nami- popote
    Popote kutazama utukufu wako
    Utukufu ulionipa, anase-ma - Bwa-na
  5. Baba si hao tu ninawaombea
    Lakini nao wale -watao-niamini
    Wote wawe umoja kama we Baba
    Ulivyo ndani yangu nami nda-ni ya-ko
  6. Sitawaacha nyinyi kama yatima
    Waipeleka roho, -yako- e Baba
    Nawe unaufanya uso wa nchi
    Uso wa nchi upya, anase-ma Bwa-na