Talanta Tulizopewa
| Talanta Tulizopewa | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Album | Nakaza Mwendo (Vol 19-20) | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | A. Manota | 
| Views | 7,462 | 
Talanta Tulizopewa Lyrics
- { Talanta tulizopewa na Mungu (Mwenyezi)
 Tuzitumieni kwa kujipatia utakatifu } *2
- Kama wewe ni baba wa familia
 Au kama wewe ni mama wa familia
 Kama wewe ni kasisi kanisani
 Au kama wewe mtawa kanisani
 Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
- Kama wewe ni hakimu toa haki
 Au kama wewe askari tenda haki
 Usionee wanyonge masikini
 Acha rushwa acha dhuluma tenda haki,
 Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
- Kama wewe dakitari au nesi
 Hudumia wagonjwa wote kwa upendo
 Mashambani maofisini wajibika
 Acha uvivu fanya kazi kwa bidii,
 Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu*2
- Viongozi na watawala tenda haki
 Kumbukeni mtaulizwa na Muumba
 Walimu nanyi fundisheni maadili
 Nanyi wafanya biashara tenda haki
 Tutaulizwa juu ya talanta alizotupa Muumba *2
 
  
         
                            