Talanta Tulizopewa

Talanta Tulizopewa
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumNakaza Mwendo (Vol 19-20)
CategoryTafakari
ComposerA. Manota
Views6,420

Talanta Tulizopewa Lyrics

  1. { Talanta tulizopewa na Mungu (Mwenyezi)
    Tuzitumieni kwa kujipatia utakatifu } *2

  2. Kama wewe ni baba wa familia
    Au kama wewe ni mama wa familia
    Kama wewe ni kasisi kanisani
    Au kama wewe mtawa kanisani
    Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
  3. Kama wewe ni hakimu toa haki
    Au kama wewe askari tenda haki
    Usionee wanyonge masikini
    Acha rushwa acha dhuluma tenda haki,
    Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
  4. Kama wewe dakitari au nesi
    Hudumia wagonjwa wote kwa upendo
    Mashambani maofisini wajibika
    Acha uvivu fanya kazi kwa bidii,
    Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu*2
  5. Viongozi na watawala tenda haki
    Kumbukeni mtaulizwa na Muumba
    Walimu nanyi fundisheni maadili
    Nanyi wafanya biashara tenda haki
    Tutaulizwa juu ya talanta alizotupa Muumba *2