Talanta Tulizopewa
Talanta Tulizopewa | |
---|---|
Choir | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha |
Album | Nakaza Mwendo (Vol 19-20) |
Category | Tafakari |
Composer | A. Manota |
Source | St. Theresa Cathedral Arusha Tanzania |
Musical Notes | |
Timesignature | 3 8 |
Musickey | C Major |
Notes | Open PDF |
Talanta Tulizopewa Lyrics
{ Talanta tulizopewa na Mungu (Mwenyezi)
Tuzitumieni kwa kujipatia utakatifu } *2
1. Kama wewe ni baba wa familia
Au kama wewe ni mama wa familia
Kama wewe ni kasisi kanisani
Au kama wewe mtawa kanisani
Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
2. Kama wewe ni hakimu toa haki
Au kama wewe askari tenda haki
Usionee wanyonge masikini
Acha rushwa acha dhuluma tenda haki,
Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu *2
3. Kama wewe dakitari au nesi
Hudumia wagonjwa wote kwa upendo
Mashambani maofisini wajibika
Acha uvivu fanya kazi kwa bidii,
Vyema utimize wajibu wako upate utakatifu*2
4. Viongozi na watawala tenda haki
Kumbukeni mtaulizwa na Muumba
Walimu nanyi fundisheni maadili
Nanyi wafanya biashara tenda haki
Tutaulizwa juu ya talanta alizotupa Muumba *2
Favorite Catholic Skiza Tunes
SMS the Skiza ID to 811 to get the song as your Skiza tune.
Title | SKIZA ID |
Cha Kutumaini Sina | 5814855 |
Roho Yangu na Ikuimbie | 5814859 |
Nikupe Nini Mungu Wangu | 7482438 |
Sasa Wakati Umefika | 7482439 |
Nitakwenda Mimi Mwenyewe | 7482440 |
Zaeni Matunda Mema | 5814860 |
Bwana Kama Wewe Ungehesabu Maovu Yetu | 7482444 |
Huniongoza Mwokozi | 5814856 |
Utukuzwe Ewe Baba | 7482441 |
Tazama Tazama | 7482442 |