Tumkimbie Shetani

Tumkimbie Shetani
Performed by-
CategoryTafakari
Views3,147

Tumkimbie Shetani Lyrics

  1. Tumkimbie (tumkimbie) huyo huyo shetani (kimbia)
    Shetani ameleta mafarakano katika dunia hii *2
    Chuki zimetawala ee Bwana, magonjwa ni mengi sana
    Tufanye nini tuepuke na matatizo haya *2

  2. Tumeyasahau maagizo ya Bwana wetu Yesu Kristu
    Aliyotufundisha sisi wanadamu, Ndiyo maana kuna machafuko
  3. Mwenye masikio na ayasikilize maneno ya Bwana
    Mkatende kama alivyotenda yeye, Dunia itakuwa na amani
  4. Tungeishi na amani kama samaki katika bahari
    Dunia hii ingekuwa ni paradise, Kama bustani ile ya Edeni
  5. Tumelia sana Bwana hata machozi hayatoki tena
    Tufanye nini sisi ni viumbe wako, Njoo haraka utusaidie