Tumkimbie Shetani
   
    
     
        | Tumkimbie Shetani | 
|---|
| Performed by | - | 
| Category | Tafakari | 
| Views | 3,539 | 
Tumkimbie Shetani Lyrics
 
             
            
- Tumkimbie (tumkimbie) huyo huyo shetani (kimbia)
 Shetani ameleta mafarakano katika dunia hii *2
 Chuki zimetawala ee Bwana, magonjwa ni mengi sana
 Tufanye nini tuepuke na matatizo haya *2
- Tumeyasahau maagizo ya Bwana wetu Yesu Kristu
 Aliyotufundisha sisi wanadamu, Ndiyo maana kuna machafuko
- Mwenye masikio na ayasikilize maneno ya Bwana
 Mkatende kama alivyotenda yeye, Dunia itakuwa na amani
- Tungeishi na amani kama samaki katika bahari
 Dunia hii ingekuwa ni paradise, Kama bustani ile ya Edeni
- Tumelia sana Bwana hata machozi hayatoki tena
 Tufanye nini sisi ni viumbe wako, Njoo haraka utusaidie