Umekosa Nini Yesu

Umekosa Nini Yesu
Alt TitleNjia ya Msalaba
Performed by-
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Views45,972

Umekosa Nini Yesu Lyrics

  1. Tuifuate Njia ya Msalaba, tuifuate mpaka Kalvari
    Tusimamapo bila haya, (msalaba *2) huponya roho

    * * * * * *
  2. Umekosa Nini we Yesu, kushtakiwa bure kwa Pilato
    Wenye kustahili hukumu, si wewe, si wewe, Bwana ni sisi
  3. Ole msalaba huo mzito, apagazwa Mwana Mpenzi wa Mungu
    Mwili waenea mateso, alipa, alipa madhambi yetu
  4. Ona Mumba Mbingu na nchi, yupo chini mzigo wamwelemea
    Na mtu kiumbe chake kwa ukali, ampiga, ampiga bila huruma
  5. Huko njiani we Maria, waonaje hali ya mwanao
    Ni damu tupu na vidonda, machozi, machozi yamfumba macho
  6. Kwa Simoni heri ya kweli, mimi pia Yesu nisaidie
    Kuchukua mzigo wa ukombozi, kuteswa, kuteswa pamoja nawe
  7. Uso wa Yesu malaika, Bethlehemu wakuabudu
    Bahati yake Veronika, kupangusa, kupangusa mfalme wa mbingu
  8. Wakimvuta huku na huku, wauaji wakamchokesha bure
    Chini wamtupa bado kwa nguvu, aibu, aibu yao milele
  9. Wanawake wa Israeli, msilie kwa sababu hiyo
    Muwalilie hao kwa dhambi, upanga, upanga ni juu yao
  10. Mwokozi sasa ni ya tatu, kuanguka chini ya msalaba
    Katika dhambi za ulegevu, nijue, nijue kutubu hima
  11. Muje malaika wa Mbingu, funikeni mwiliwe kwa huruma
    Vidonda vyake na utupu, askari, askari wamvulia
  12. Hapo mkristu ushike moyo, Bwana wako alazwa msalabani
    Mara miguu na mikono, yafungwa, yafungwa kwa misumari
  13. Yesu mpenzi nakuabudu, msalabani unapohangaika
    Nchi yatetemeka kwa hofu, na jua, na jua linafifia
  14. Mama Maria mtakatifu, upokee maiti ya mwanao
    Tumemwua kwa dhambi zetu, twatubu, twatubu kwake na kwako
  15. Pamoja naye kaburini, zika dhambi na ubaya wa moyo
    Yesu tuwe wakristu wa kweli, twakupa, twakupa sasa mapendo

    * * * * * * * * *
  16. Katika roho yangu Bwana, chora mateso niliyokutesa
    Nisiyasahau madeni, na kazi, na kazi ya kuokoa