Watu Hawatalingana
| Watu Hawatalingana | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya ya Moyo Safi wa Bikira Maria, Unga Limited Arusha | 
| Album | Watu Hawalingani | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | Fr. A. Msigwa | 
| Views | 6,772 | 
Watu Hawatalingana Lyrics
- {Watu hawatalingana (daima), watatofautiana
 (nayo ni) makusudi yake Mungu, jina lake litukuzwe } *3{ Sote tumeumbika tulivyo (kadiri) ya mapenzi yake Mungu
 Ili utukufu wake Mungu (Mwenyezi) ujulikane kwa wote } *2
- Kweli wanadamu wote (hakika) tumeumbwa kwa udongo
 (hivyo) asili yetu ni moja, tumetoka mavumbini
- Wapo walio wanyonge (lakini), pia wapo wenye nguvu
 (kusudi) Mungu kawaumba hivyo, ili wahudumiane
- Wengine kawabariki (sana), amewajalia mali
 (lakini) wengine amewashusha, wamekuwa hohe hahe.
- Wale walio tajiri (kamwe), wasiwanyime fukara
 (kwani) maskini wahitaji, huruma ya matajiri
- Wote tu wana wa Mungu (hivyo) tuonyeshane upendo
 (ili) Mungu wetu atukuzwe, sasa na hata milele.
Baadhi ya kwaya ambazo zimerekodi wimbo huu ni
* Kwaya ya Moyo Safi wa Bikira Maria, Unga Limited Arusha (Watu Hawalingani album)
* Kwaya ya Mt. Vincenti Palloti Makiungu Dsm (Wema Mkamilifu album)
* Kwaya ya Mt. Paulo, Chuo Kikuu cha Nairobi (Ikatetemeka Nchi album)
  
 
 
 
  
         
                            