Watumishi Wake Baba
| Watumishi Wake Baba | |
|---|---|
|  | |
| Performed by | - | 
| Category | Kwaresma na Toba (Lent & Repentance) | 
| Composer | (traditional) | 
| Video | Watch on YouTube | 
| Views | 63,627 | 
Watumishi Wake Baba Lyrics
- Watumishi wake Baba wangapi waliopo
 Wanakula na kusaza chakula chake BabaNami - Nami nataabika hapa
 Nashi - Nashiriki na nguruwe
 Chaku - Chakula kisichofaa, yanipasa kurudi
 Nita - Nitarudi na kusema
 Baba - Baba yangu nisamehe
 Nime - Nimekosa kwake Mungu, na mbele yako Baba
- Baba kamwona yu mbali kashikwa na huruma
 Akakimbia kumlaki kamkumbata na busu
- Baba sistahili tena kuitwa mwana wako
 Unifanye kama mmoja wa watumishi wako
- Baba yangu nimekosa ninaomba huruma
 Unisamehe nirudi nikakutumikie
- Wanikaribisha mimi kwenye karamu yako
 Meza imeandaliwa inaningoja mimi
- Nasogea ninakuja ninakukimbilia
 Mimi ni mtoto mpotevu Baba unipokee
 
  
         
                            