Yesu wa Vituko

Yesu wa Vituko
Performed bySt. Joseph Migori
AlbumNimeteuliwa
CategoryKristu Mfalme (Christ the King)
ComposerAlfred Ossonga
Views10,624

Yesu wa Vituko Lyrics

  1. Huyu ndiye Yesu wa miujiza nauliza
    Huyu ndiye Yesu wa maajabu nauliza
    Aliyegeuza maji kuwa divai
    Kwenye harusi kule Kana Galilaya

    Huyu ndiye Yesu, (Yesu) Mwana Wa Mungu
    Huyu ndiye Yesu, (Yesu) kutoka Mbinguni
    Huyu ndiye Yesu, aliyekuja kwetu
    Huyu ndiye Yesu mwenye upendo mwingi

  2. Huyu ndiye Yesu Mnazareti nauliza
    Huyu ndiye Mwana wa seremala nauliza
    Aliyewaita wavuvi wa samaki
    Akawageuza wavuvi wa watu
  3. Huyu ndiye Yesu mwenye huruma nauliza
    Huyu ndiye Yesu Simba wa Yuda nauliza
    Aliyewakemea mapepo kwa nguvu
    Aliyewaamuru mapepo watoke
  4. Huyu ndiye Yesu mwenye baraka nauliza
    Huyu ndiye Yesu mwenye chakula nauliza
    Aliyewalisha watu elfu tano
    Kwa mikate mitano na samaki wawili
  5. Huyu ndiye Yesu mwenye vituko nauliza
    Huyu ndiye Yesu asiyeshindwa nauliza
    Aliyewatimua watu hekaluni
    Walipogeuza hekalu kuwa soko
  6. Huyu ndiye Yesu mwenye hekima nauliza
    Huyu ndiye Yesu mwenye elimu nauliza
    Aliyeng'amua hila zake shetani
    Pale nyikani alipojaribiwa