Tumuogope Mungu

Tumuogope Mungu
Performed bySt. Don Bosco Mirerani
AlbumRamani ya Mbinguni
CategoryTafakari
ComposerE. F. Jissu
Views4,978

Tumuogope Mungu Lyrics

  1. { Ni nani mwanadamu mwenye nguvu kuliko Mungu (hakuna) } *2
    Ajitokeze mbele za watu tumuone, hakuna
    Iyelele iyele, iyelele iyele - hakuna *4
    Ni Mungu tu awezaye yote hivyo tumwogope

  2. Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote
    Analopanga Mungu mwanadamu halipangui
    Akipanga uwe padri, utakuwa wewe padri
    Akipanga we mtawa, utakuwa we mtawa, muogope Mungu
  3. Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote
    Analopanga Mungu mwanadamu halipangui
    Akipanga uwe raisi, utakuwa we rais
    Akipanga uwe waziri, basi wewe ni waziri, muogope Mungu
  4. Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote
    Analopanga Mungu mwanadamu halipangui
    Akipanga uwe mbunge, basi wewe ni mbunge
    Akipanga uwe balozi, utakuwa we balozi, muogope Mungu
  5. Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote
    Analopanga Mungu mwanadamu halipangui
    Akipanga uwe tajiri, basi wewe ni tajiri
    Akipanga uwe maskini, utakuwa maskini, muogope Mungu
  6. Huu ndio ukweli kwa wanadamu wote
    Analopanga Mungu mwanadamu halipangui
    Akipanga kukurudisha, mavumbini utarudi
    Analopanga Mwenyezi, daima halipingiki, muogope Mungu