Baba Mama na Watoto

Baba Mama na Watoto
Performed bySt. Cecilia Zimmerman
AlbumNitayasimulia Matendo (Vol 6)
CategoryFamilia
ComposerT. B. Pamera
Views9,231

Baba Mama na Watoto Lyrics

  1. Baba mama na watoto wao ni familia kamili
    Na hawa wote ni muhimu, kujenga kanisa la Yesu
    Katika kujenga Kanisa la Yesu ujenzi huanza nyumbani
    Na kupeana majukumu, kila mmoja na lake

    Mama awe katekista, na baba awe padre
    Mama awe katekista, na baba awe padre
    {Watoto wawe ubao[ubao] kufundishia wengine
    Ili wengineo wajifunze, kuishi maisha mema} *2

  2. Mama awe katekista maana yeye ndiye mwalimu
    Kwa kuwa ana huruma na ni mlezi wa watoto
    Awafundishe mema yote, upendo sala na bidii
    Na kuwafundisha nidhamu kwa wenyewe na kwa wengine
  3. Baba yeye awe padre, tena yeye ndiye mchungaji
    Ashirikiane naye mama, watoto wao kuwalea
    Awe mwelekezaji pale watoto wanapopotoka
    Ili waweze kujenga familia iliyo bora
  4. Watoto wawe ubao ubao, kufundishia wengine
    Kwa tabia zao nzuri na uadilifu mwema
    Watakuwa ni mfano bora na kielelezo sawia
    Hiyo ndiyo familia ya kumpendeza Mungu

    Baba mama na watoto wao ni familia kamili
    Na hawa wote ni muhimu, kujenga kanisa la Yesu
    Katika kujenga Kanisa la Yesu ujenzi huanza nyumbani
    Na kupeana majukumu, kila mmoja na lake