Tukeshe

Tukeshe
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumKidole Juu (Vol 23)
CategoryTafakari
ComposerP. F. Mwarabu
Views6,895

Tukeshe Lyrics

  1. Tukeshe - Tukeshe sote kila wakati
    Tukimwomba Mungu atupe Baraka zake
    Tukeshe - Tukeshe tukeshe kila wakati
    Tukimwomba Yesu atufikishe Mbinguni

  2. [s] Na tukeshe kama wale wanawali
    Waliozijaza taa zao mafuta
  3. [t] Tukeshe tukiomba kwa moyo wote
    Tuupate uzima wa milele
  4. Watu wote tukeshe siku zote
    Tuziweke hazina mbinguni
    Siku ya mwisho tufike kwake Mungu
    Tuishi naye milele milele
  5. Dunia hii ni shida na mateso
    Tusidanganywe na raha za muda
    Ona dhambi maovu na magonjwa
    Yanatisha tena yahuzunisha
  6. Tujikane tutubu tuungame
    Tujaliwe huruma yake Mungu
    Tusali sana tuombe neema zake
    Tuwe tayari siku ya hukumu