Mwimbieni Bwana Zaburi
| Mwimbieni Bwana Zaburi | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Album | Kidole Juu (Vol 23) | 
| Category | Entrance / Mwanzo | 
| Composer | G. Tesha | 
| Views | 7,625 | 
Mwimbieni Bwana Zaburi Lyrics
- Mwimbieni Bwana zaburi
 Mwimbieni kwa kinubi) *2
 {Mwimbieni kwa kinubi na sauti ya zaburi
 Mwimbieni kwa panda na sauti ya baragumu (wote)
 Shangilieni mbele za mfalme Bwana wa majeshi}
- Bahari na ivume na vyote viijazavyo,
 Ulimwengu na wote wanaokaa ndani yake
 Milima naiimbe kwa furaha mbele za Bwana Mungu
- Wanyama wa mwituni na mimea ya kondeni
 Upepo na uvume kupeleka habari hizi
 Kwa ndege wa angani na viumbe vilivyo baharini
- Nikitazama kushoto kulia nyuma na mbele
 Nikitazama angani nikitazama ardhini
 Kila nionacho kinasimulia utukufu wako
- Kwa maana mbingu na dunia ni kazi yako
 Jua na mwezi na nyota anga pia nayo mawingu
 Ni kazi ya vidole vyako na ujuzi wa mikono yako
 
  
         
                            