Mwimbieni Bwana Zaburi

Mwimbieni Bwana Zaburi
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumKidole Juu (Vol 23)
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerG. Tesha
Views6,625

Mwimbieni Bwana Zaburi Lyrics

  1. Mwimbieni Bwana zaburi
    Mwimbieni kwa kinubi) *2
    {Mwimbieni kwa kinubi na sauti ya zaburi
    Mwimbieni kwa panda na sauti ya baragumu (wote)
    Shangilieni mbele za mfalme Bwana wa majeshi}

  2. Bahari na ivume na vyote viijazavyo,
    Ulimwengu na wote wanaokaa ndani yake
    Milima naiimbe kwa furaha mbele za Bwana Mungu
  3. Wanyama wa mwituni na mimea ya kondeni
    Upepo na uvume kupeleka habari hizi
    Kwa ndege wa angani na viumbe vilivyo baharini
  4. Nikitazama kushoto kulia nyuma na mbele
    Nikitazama angani nikitazama ardhini
    Kila nionacho kinasimulia utukufu wako
  5. Kwa maana mbingu na dunia ni kazi yako
    Jua na mwezi na nyota anga pia nayo mawingu
    Ni kazi ya vidole vyako na ujuzi wa mikono yako