Asante Kwa Wema
| Asante Kwa Wema | |
|---|---|
| Performed by | Kwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha | 
| Album | Kidole Juu (Vol 23) | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | Single | 
| Views | 20,687 | 
Asante Kwa Wema Lyrics
- Bwana alinitendea mambo makuu
 Nilipoita jina lake aliniitikia
 Alinitegemeza katika taabu zangu{ Asante- kwa wema wako
 Asante-kwa ukarimu
 Asante kwa pendo lako nashukuru } * 2
- Bwana ameniponya na magonjwa mengi
 Pia amenikinga na ajali mbaya sana
 Amenitoa katika mitego ya shetani
- Nimetafakari upendo wake Bwana
 Kujivika ubinadamu na kufa msalabani
 Ili nikombolewe utumwani wa shetani
- Ni mara nyingi sana nimetenda dhambi
 Lakini Bwana Yesu hakunihukumu kwa dhambi
 Hakuna kama Bwana yeye ni Mungu pekee
- Wema wake Mungu wangu hauna mwisho
 Ameniandalia makao baada ya kifo
 Masharti yake niwe nimetii amri za Mungu
- Enyi ndugu zangu mlio katika Kristu
 Unganeni pamoja nami kumshukuru Mungu
 Ni mema mengi sana yeye ametujalia
 
  
         
                            