Asante Kwa Wema

Asante Kwa Wema
Performed byKwaya Kuu ya St. Cecilia Arusha
AlbumKidole Juu (Vol 23)
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerSingle
Views16,712

Asante Kwa Wema Lyrics

  1. Bwana alinitendea mambo makuu
    Nilipoita jina lake aliniitikia
    Alinitegemeza katika taabu zangu

    { Asante- kwa wema wako
    Asante-kwa ukarimu
    Asante kwa pendo lako nashukuru } * 2

  2. Bwana ameniponya na magonjwa mengi
    Pia amenikinga na ajali mbaya sana
    Amenitoa katika mitego ya shetani
  3. Nimetafakari upendo wake Bwana
    Kujivika ubinadamu na kufa msalabani
    Ili nikombolewe utumwani wa shetani
  4. Ni mara nyingi sana nimetenda dhambi
    Lakini Bwana Yesu hakunihukumu kwa dhambi
    Hakuna kama Bwana yeye ni Mungu pekee
  5. Wema wake Mungu wangu hauna mwisho
    Ameniandalia makao baada ya kifo
    Masharti yake niwe nimetii amri za Mungu
  6. Enyi ndugu zangu mlio katika Kristu
    Unganeni pamoja nami kumshukuru Mungu
    Ni mema mengi sana yeye ametujalia