Johera
Johera Lyrics
Johera ( dakunyi's herahera)*2
Manyase endwaro wololo hawawene
Johida (dakunyi's hidahida )*2
Manyase endwarowololo niwakadhi
Njooni wote tushangilie,
{Tuimbe kwa furaha, tucheze bila mwisho,
Tutoe shukrani kwa Bwana mtawala }*2
- Waumini simameni, mbele zake Mungu wetu
Waimbaji mziimbe, sifa zake Jehova Rama
Waumini tamkeni, utukufu wake Yahweh
Makasisi na watawa na wacheze nyumbani mwake
shangwe
- Kwa sauti ya kinanda, kwa filimbi na kayamba
Kwa kinubi na kwa zeze, tunamwimbia Mungu wetu
Kwa kelele za furaha, kwa makofi kwa machezo
Kwa vigelegele kweli, njooni nyote tutoe shukrani
- Mwimbieni Mungu wetu, mwimbieni wimbo mpya
Mwimbieni kwa furaha mwimbieni kwa shangwe kubwa
Mungu wetu ni mkuu, ametenda maajabu
Ameumba vitu vyote, ulimwengu na jeshi lake lote
- Mungu wetu katuumba, ili sote tumjue
Sisi sote tumpende, tumtumikie daima
Ametupa vitu vyote,atulinda siku zote
Tuna heri ya milele, tutaishi mbinguni kwake Baba