Johera

Johera
Performed bySt. Joseph Migori
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerAfred Ossonga
Views9,754

Johera Lyrics

  1. Johera ( dakunyi's herahera)*2
    Manyase endwaro wololo hawawene
    Johida (dakunyi's hidahida )*2
    Manyase endwarowololo niwakadhi
    Njooni wote tushangilie,
    {Tuimbe kwa furaha, tucheze bila mwisho,
    Tutoe shukrani kwa Bwana mtawala }*2

  2. Waumini simameni, mbele zake Mungu wetu
    Waimbaji mziimbe, sifa zake Jehova Rama
    Waumini tamkeni, utukufu wake Yahweh
    Makasisi na watawa na wacheze nyumbani mwake
    shangwe
  3. Kwa sauti ya kinanda, kwa filimbi na kayamba
    Kwa kinubi na kwa zeze, tunamwimbia Mungu wetu
    Kwa kelele za furaha, kwa makofi kwa machezo
    Kwa vigelegele kweli, njooni nyote tutoe shukrani
  4. Mwimbieni Mungu wetu, mwimbieni wimbo mpya
    Mwimbieni kwa furaha mwimbieni kwa shangwe kubwa
    Mungu wetu ni mkuu, ametenda maajabu
    Ameumba vitu vyote, ulimwengu na jeshi lake lote
  5. Mungu wetu katuumba, ili sote tumjue
    Sisi sote tumpende, tumtumikie daima
    Ametupa vitu vyote,atulinda siku zote
    Tuna heri ya milele, tutaishi mbinguni kwake Baba