Pilka Pilka
   
    
     
         
          
            Pilka Pilka Lyrics
 
             
            
- Pilka pilka kila siku watu wa dunia
 Wanahangaika kutafuta mali za dunia
 Asubuhi ni msongamano, mchana vilevile
 Usiku shughuli zafanyika kama kawaida
 
 Tafuteni kwanza ufalme ule wa mbinguni
 Na hayo mengine (hakika) mtazidishiwa
 {Yeye Mungu (Mwenyezi) mtetezi (ajabu)
 Mkiamini atawashughilikia } * 2
- Pilika pilika watu wengi kutafuta elimu
 Hawakumbuki kwamba Yesu ni mwalimu tosha
 Ajali nyingi barabarani zinafanyika kwetu
 Tumesahau kwamba Yesu ni dereva tosha
- Pilika pilika twatafuta hospitali kubwa
 Huku daktari mkuu ni Mungu wa majeshi
 Watu watafuta waganga ili wapate mali
 Bali Mungu wa mbinguni ndiye mmliki wa vyote
- Pilika pilika tunawaza usiku na mchana
 Vile tutakula vizuri na kuvaa vizuri
 Kwani ndege wale wa angani wanalishwa na nani
 Kama siyo Mungu wa mbinguni basi huyo nani
- Pilika pilika wenzangu tumuelekee Mungu
 Tusifadhaike bali tuwe na matumaini
 Atatujalia mema mengi tukiwa duniani
 Mwisho tutafurahi na Yesu kule juu mbinguni