Nyamazeni Sasa

Nyamazeni Sasa
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumNyumba ya Roho
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views6,709

Nyamazeni Sasa Lyrics

  1. {He he! he he! Nyamazeni sasa mkae kimya,
    (nyamazeni) nyamazeni sasa mkae kimya! }*2
    Nendeni mkajifunze upendo nenda
    (nenda ndugu) Kapunguzeni maneno mengi
    (mengi tena) Acheni ufarisayo kando
    (kando Kisha) Mkajifunze upendo nenda

  2. Kulitajataja jina la Yesu, na kutolitaja taja kabisa
    Yote ni sawa kabisa mmmh mmh
    Lililo la muhimu, upendo,
    Kuvumilia yote, upendo
    Kuamini yote, upendo,
    Kutumaini yote, upendo
  3. Kusudi watu wasiwatambue kwa yale mnayosema
    Kwa yale maneno, bali kwa matendo tu
    Kwa kuwathamini na kuwajali wenzenu daima *2
    Kwa kuwakumbuka wale walio wadogo na wanyonge
    Kwa kuwakumbuka wale walio wadogo na!
    he! he! upendo! *3 he! upendo