Tanzania

Tanzania
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumMungu Yule
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views9,265

Tanzania Lyrics

  1. Mwenyezi Mungu Rahimu na mradhi mwema,
    salamu salamu Mwumba wa Adamu
    Watanzania tumekuja kwa wimbo,
    na tenzi kuongea nawe leo hii
    Uchaguzi mkuu huu tunaoandaa,
    twaomba ujae baraka zako kuu
    Kusudi uwepo wako udhihirike,
    katika serikali tutakayounda
  2. Rais mpya awe fimbo bora,
    awe taa ya kweli kwenye kinara
    Wabunge wawe matawi mazuri,
    yenye kuzaa kwenye mti wa rutuba
    Madiwani wawe watu wa watu,
    kuongoza watu kwa ajili ya watu
    Tujenge Tanzania madhubuti,
    mioyoni badala ya ardhini
  3. Wagonjwa wapone, makiwa wafarijiwe,
    masikini waonje maziwa kila siku
    Wajane waishi, yatima waende shule,
    fukara waone thamani ya utu wao
    Majanga yakome, majeruhi watibiwe,
    walio gerezani wawe huru mitaani
    Undugu ukue, amani iongezeke,
    na wahalifu wote wabadilishe tabia
  4. Na watoto, watoto wadogo,
    walelewe kwa maadili
    Madhehebu, yote ya kidini,
    yawe tahadhari ya upendo
    Navyo vyama, vyetu vya siasa,
    viwe siri kuu ya amani
    Ibilisi, afunge virago,
    aondoke kamwe asirudi!
  5. Kiapo atakachoapa rais mpya,
    kidumu hata hatimamu ya dahari
    Majaribu yote yatakayotukumbuka,
    yapimwe yasizidi kimo chetu
    Mwenyezi Mungu rahimu twakuomba,
    tulinde tulinde bila ya kuchoka
    Ili mwisho wa safari ya hapa,
    tufike mbinguni wote Tanzania