Siri ya Mafanikio

Siri ya Mafanikio
Performed byBMT Ledochowska K/Ndege Dodoma
AlbumDawa ya Uzima
CategoryTafakari
Views4,236

Siri ya Mafanikio Lyrics

  1. Nikateleza nikatapatapa,
    sauti ile ikanirudia tena
    Ikanambia usiwe na hofu,
    inua macho yako kwenye mti huu (na kisha)

    Tazama tundu hili takatifu la neema
    Kwenye moyo uliojaa pendo
    Na ndilo siri ya mafanikio ya maisha
    Ya furaha na amani ya kweli (aleluya)
    Wa Yesu umefunuliwa moyo huo
    Nauona uko wazi moyo ( tukufu)
    Unanimiminia neema moyo huo
    Uko wazi uko wazi moyo

  2. Ulipochomwa kwa chuma kigumu,
    na ni ugumu ule wa mioyo yetu
    Ukatujibu kwa kumwaga maji,
    maji laini nayo damu ya sadaka (lakini)
  3. Hauchukii hauna kisasi,
    moyo mpole mwema na mnyenyekevu
    Shida na tabu tukiukabidhi,
    unachotoa ni neema na ushindi
  4. Mahangaiko na kumaka kwetu,
    tuupelekee moyo wake Yesu
    Tutafurahi tutafanikiwa,
    damu na maji yake yatatutakasa (lakini)
  5. Ili daima atukuzwe Baba,
    na mwana atukuzwe Roho Mtakatifu
    Ilivyokuwa toka kule mwanzo,
    sasa na siku zote daima milele (amina)