Duka la Shetani
| Duka la Shetani | |
|---|---|
| Alt Title | Usipange Foleni | 
| Performed by | St. Veronica Kariakor Dar-es-salaam | 
| Album | Kama Nyuki | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | Victor Aloyce Murishiwa | 
| Views | 6,675 | 
Duka la Shetani Lyrics
- Usipange foleni kwenye duka la shetani
 Utauziwa dhambi faida yake mauti
 Nenda ukajipange dukani kwa Bwana Yesu
 Utapata kibali cha kuingia mbinguni
- Enyi wavuta bangi, na madawa ya kulevya
 Mbona mmejipanga katika duka la shetani
- Na ninyi wala rushwa, makahaba na wachawi
 Mbona mmejipanga katika duka la shetani
- Duka lake shetani limejaa vitu vingi
 Tena vyapendeza sana na kuuvutia moyo
- Ramani ya mbinguni nenda kwake Yesu
 Ramani ya kuzimu shetani ndiye mchoraji
- Mnaofunga ndoa katika jinsia moja
 Nanyi mmejipanga katika duka la shetani
- Mavazi ya aibu dada zetu mwajivika
 Mnaita vimini shetani anachekelea
 
  
         
                            