Yesu Kanikuta Jangwani

Yesu Kanikuta Jangwani
Performed byOur Lady of Guadalupe
CategoryKwaresma na Toba (Lent & Repentance)
Composer(traditional)
Views20,041

Yesu Kanikuta Jangwani Lyrics

  1. Yesu kanikuta jangwani, akaniambia, nenda huko Yerusaleme
    Yesu kanikuta gizani, akasema, kimbilia Yerusaleme

    Mimi ni kipofu ni mauti (mimi ni mauti)
    Mimi ni kipofu sioni (mimi sioni)
    { Kulikuwa giza, kukapambazuka
    Nikamwona Bwana Bwana wangu }*2

  2. Natamani mji ule, Yerusaleme kuna nuru kuna raha
    Dhambi zangu matendo yangu, ni maovu, tazameni msalabani

    Upindo wa nguo (nguo yako safi)
    Upindo wa nguo (nguo yako nzuri)
    { Uniguse moyo, moyoni mwangu
    Nitaimba sifa sifa zako } *2

  3. Watakatifu wa moyo, tumsifuni, Bwana mwenye nchi na mbingu
    Twende huko nchi ya mbali, ya Kanaani ndiko tutaishi milele

    { Fimbo yake Musa ilituokoa
    Fimbo yake Musa, ilituongoza
    { Nchi ile ya Misri (nchi ya farao)
    Tulimwona Bwana mwenye enzi } }*2