Milele Milele Msifuni

Milele Milele Msifuni
Performed byManzese
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerM. B. Syote
Views6,042

Milele Milele Msifuni Lyrics

  1. Milele milele msifuni Bwana
    Na ahimidiwe Bwana milele,
    Amina, amina, aleluya
    Rehema za Bwana ni za milele
    Na uaminifu wa Mungu wetu,
    Ni kwa vizazi hata vizazi

    { Njooni, tuimbe, tumwimbie Bwana
    Yeye (ndiye) wokovu, wokovu wetu (Bwana)
    Ni Mungu wetu na mwumba wetu, aleluya aleluya } *2

  2. Nitakushukuru ee Bwana Mungu
    Nitalishukuru jina la Bwana,
    Ee Bwana mfalme Mungu wangu
    Pigeni vigelegele pigeni
    Pigeni magoti mbele za Bwana
    Kwa maana ndiye Mungu wetu
  3. Atawabariki wamchao Bwana
    Wadogo wakubwa awabariki
    Msaada wao na ngome yao
    Tazama atabarikiwa hivyo
    Atabarikiwa amchaye Bwana
    Awabariki toka Sayuni