Shukrani Yangu

Shukrani Yangu
Alt TitleHii Sio Hadithi
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumUshuhuda Tosha
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerJ. C. Shomaly
Views5,251

Shukrani Yangu Lyrics

  1. Hii sio hadithi ninataka kusimulia
    Wala sio historia wala si somo la siasa
    Ni mambo mema sana aliyotenda Mungu kwangu
    Na nisipoyatamka nitakuwa sina fadhila

    Wazazi wamenilea mpaka nimefika hapa
    Majirani na ndugu zangu pia wamenipiga jeki
    [ b ] Baba usikie sala hii mimi natoa

    { Wabariki wazazi wangu wape maisha marefu
    Wabariki na ndugu zangu wape amani tele
    Marafiki zangu pia mimi mwenyewe
    Siwezi kusahau kuwaombea na adui zangu } *2

  2. Mungu ninakushukuru, afya njema wanijalia
    Kila ninapoamka sijui nitakupa nini
    Masomo yangu nasoma pia ninafaulu vyema
    Sasa nimefika hapa sio kwamba mimi ni mwema
  3. Shuleni niliposoma nilikuwa na marafiki
    Waliosoma vizuri pia na wenye afya njema
    Sio wote waliweza kufikia nilipofika
    Nashindwa niseme nini jinsi umenipenda mimi
  4. Vijijini nimeishi watu wengi nimewaona
    Hawana mbele na nyuma wameishia kunywa pombe
    Maisha yao magumu elimu yao haba haba
    Nashindwa nikupe nini hapa nilipofika mimi
  5. Siwezi kusema mengi najua wewe ndiwe kinga
    Nibariki nijalie maisha yenye kupendeza
    Kipaji nilicho nacho cha kuimba na kuhubiri
    Kiwavute watu wengi wakuabudu wewe Bwana