Ushuhuda Tosha
| Ushuhuda Tosha | |
|---|---|
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Ushuhuda Tosha | 
| Category | Thanksgiving / Shukrani | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 6,916 | 
Ushuhuda Tosha Lyrics
- Tuna haki ya kutamka na kutoa ushuhuda
 Mambo mema alotenda Mungu pia na kwa huruma
 Ninamwambia naye jirani Mungu ana huruma{ Ushuhuda, huo ni ushuhuda tosha (nasema)
 Ni huruma, Mungu ana huruma nyingi (hakika)
 Ninapolala pia ninaamka huo wote ni ushuhuda tosha } *2
- Kaumba mbingu na dunia wanyama hata samaki
 Binadamu na akili nyingi sisi tukawatawale
 Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
- Tunalala bila kuomba hatimaye twaamka
 Mungu wetu na hakasiriki bado atupa mkate
 Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
- Maisha yetu twayapanga nayo yanafanikiwa
 Mara nyingi hata hatuombi kumshirikisha Mungu
 Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
- Tunapofanya biashara uongo tunatumia
 Twazikiuka amri za Mungu ili tupate faida
 Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
- Ni mengi hatujatamka wanadamu tunafanya
 Tunaomba msamaha Mungu sisi sote walegevu
 Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
 
  
         
                            