Ushuhuda Tosha

Ushuhuda Tosha
Performed bySt. Paul Students' Choir (University of Nairobi)
AlbumUshuhuda Tosha
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerJ. C. Shomaly
Views5,975

Ushuhuda Tosha Lyrics

  1. Tuna haki ya kutamka na kutoa ushuhuda
    Mambo mema alotenda Mungu pia na kwa huruma
    Ninamwambia naye jirani Mungu ana huruma

    { Ushuhuda, huo ni ushuhuda tosha (nasema)
    Ni huruma, Mungu ana huruma nyingi (hakika)
    Ninapolala pia ninaamka huo wote ni ushuhuda tosha } *2

  2. Kaumba mbingu na dunia wanyama hata samaki
    Binadamu na akili nyingi sisi tukawatawale
    Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
  3. Tunalala bila kuomba hatimaye twaamka
    Mungu wetu na hakasiriki bado atupa mkate
    Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
  4. Maisha yetu twayapanga nayo yanafanikiwa
    Mara nyingi hata hatuombi kumshirikisha Mungu
    Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
  5. Tunapofanya biashara uongo tunatumia
    Twazikiuka amri za Mungu ili tupate faida
    Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu
  6. Ni mengi hatujatamka wanadamu tunafanya
    Tunaomba msamaha Mungu sisi sote walegevu
    Kwa kweli Mungu ana huruma kwetu binadamu