Jeshi la Malaika
| Jeshi la Malaika | |
|---|---|
| Alt Title | Jina Kuu | 
| Performed by | St. Paul Students' Choir (University of Nairobi) | 
| Album | Ushuhuda Tosha | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | J. C. Shomaly | 
| Views | 5,446 | 
Jeshi la Malaika Lyrics
- Sasa jeshi la malaika lashangilia jina hili tukufu
 Na sisi viumbe duniani twashuhudia utukufu mkuu
 Twaungana na malaika tukisifu sana jina hili ni kuu
 Tangu Yohane atabiri na sisi sote hatuliasi ni kuuTwimbe twimbe tumsifuni Yesu, jina lake latenda makuu
 Mfalme Kristu mwana wake Mungu
 Tumsifuni tumsifuni tumshukuru Mungu
- Dhambi yake Adamu babu na bibi Eva ilikuwa asili,
 Mkombozi Yesu katumwa dunia yote sisi kutuokoa
 Waliokuwa na kiburi ni ibilisi na wenye shingo ngumu
 Wamebaki midomo wazi wakiteketea kwa moto mkali
- Wasioamini na wasiomkubali kwao ni kama ndoto,
 Muda wao ukishapita kilio chao mavuno ni mkaa
 Mawazo yao duni sana na mbinu zao zisizoenda mbali,
 Wasiokubali ya kuwa Mungu ndiye mweza wa kila kitu
- Kina Baba mama vijana pia watoto jueni hili jambo
 Dunia yote ina mwisho ya duniani ni ya muda mfupi
 Biashara zisiwe nyingi mkasahau aliyetuumba sisi,
 Mwenye uwezo wa kutoa pumzi na afya yapaswa tumtii
 
  
         
                            