Shukrani ya Mwili

Shukrani ya Mwili
Performed bySt. Don Bosco Mirerani
AlbumRamani ya Mbinguni
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views3,375

Shukrani ya Mwili Lyrics

  • Nimeunakishi mwili wangu kwa marashi na kwa saluni
    Na nimeulisha chakula safi na ukashiba
    Nimehangaika kuupamba - kwa mavazi ya kupendeza
    Na nikaunywesha kila kinywaji ukaburudika

    Tazama shukrani ya mwili huu ni uchovu na ugonjwa
    Shukrani ya mwili kwangu ni usingizi
    Shukrani ya mwili huu ni kutorithika kamwe
    Shukrani ya mwili kwangu ni kurudi mavumbini, milele
    Milele milele hazina yangu mbinguni (kweli) *4


    Nimeuhifadhi kwenye nyumba ya kifahari na geti kubwa
    Na nikaajiri mlinzi bora wa kulinda nchi
    Nimeuhifadhi kwa mashuka chandarua na makapeti
    Na nikaulaza kwenye gondoro yenye raha tupu
  • Nimeushibisha kwa anasa na starehe za kila namna
    Na hata zile zinazotumia mwili wa wengine
    Nimeukusanyia kiburi cha ujanja na ujuaji
    Na nikaupatia utukufu machoni pa watu