Misa Amecea

Misa Amecea
Performed by-
AlbumMisa Amecea
CategoryMisa (Sung Mass)
ComposerO. Kajwang
Views37,117

Misa Amecea Lyrics

BWANA UTUHURUMIE (MISA AMECEA)

  1. [ s/a ] { Bwana utuhurumie (ee Bwana)
    [ w ] Bwana utuhurumie } *2
  2. [ t/b ] { Kristu utuhurumie (ee Kristu)
    Kristu utuhurumie } *2
  3. [ s/a ] { Bwana utuhurumie (ee Bwana)
    Bwana utuhurumie } *2

UTUKUFU KWA MUNGU (AMECEA)

  1. [ t ] Utukufu kwa Mungu juu Mbinguni
    [ w ] Na amani kote duniani
    ( Kwa watu ) wenye mapenzi mema

    Tunakusifu Baba, tunakuheshimu,
    Twakuabudu sisi tunakutukuza

  2. Twakushukuru Mungu kwa tukufu
    Wako mkuu ewe Mungu mfalme
    (Ee Baba) wa Mbingu Baba yetu
  3. Bwana wetu Mwokozi Yesu Kristu
    Mwana wa pekee wake Mungu
    (Uliye) Mwanakondoo wa Mungu
  4. Unayeziondoa dhambi zote
    Za dunia utuhurumie
    (Pokea) pokea ombi letu
  5. Wewe unayeketi kuume
    Kwake Baba utuhurumie
    (Sikia) sikia ombi letu
  6. Kwani pekee yako ndiwe Bwana
    Peke yako mkuu na mkombozi
    (Pekee) pekee Yesu Kristu
  7. Kwa umoja wa Roho Mtakatifu
    Ndani yake Baba watukuzwa
    (Ee Yesu) milele na milele

NASADIKI KWA MUNGU (MISA AMECEA)

  1. Nasadiki kwa Mungu mmoja - mimi nasadiki
    Ndiye Baba yetu mwenyezi -
    Mwumba mbingu pia dunia
    Nasadiki kwa Yesu Kristu
  2. Mwana wa pekee wa Mungu -
    Aliyezaliwa kwa Baba -
    Akapata mwili kwa Roho -
    Kazaliwa naye bikira -
  3. Kisha yeye kasulubiwa -
    Kwa mamlaka yake Pilato -
    Kwa ajili yetu kateswa -
    Alikufa na akazikwa -
  4. Kafufuka katika wafu -
    Akapaa juu Mbinguni -
    Ameketi kuume kwake -
    Mungu Baba yetu Mwenyezi -
  5. Ndipo atakapotokea -
    Ili awahukumu wote -
    Kwake Roho Mtakatifu -
    Kwa kanisa la Katoliki -
  6. Ushirika wa watakatifu -
    Ondoleo la dhambi zetu -
    Nangojea ufufuko wa miili -
    Na uzima wa milele -

MTAKATIFU ( MISA AMECEA)

  • [ t ] Mtakatifu Mtakatifu Bwana - Mungu wa majeshi
    [ s ] Mtakatifu Mtakatifu Bwana - Mungu wa majeshi
  • Mbingu na dunia zimejaa zimejaa,
    Mbingu na dunia zimejaa utukufu wako *2

    Hosanna juu, hosanna juu *2 mbinguni


    Mbarikiwa nayekuja
    Mbarikiwa nayekuja mbarikiwa
    Mbarikiwa nayekuja kwa jina, jina lake Bwana

FUMBO LA IMANI ( MISA AMECEA)

  • Yesu Kristu alikufa, Yesu Kristu kafufuka
    (Yesu) Kristu atakuja, atakuja kwetu tena

MWANAKONDOO WA MUNGU (MISA AMECEA)

  1. [ t ] Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi
    Za dunia ee mwana utuhurumie
  2. [ s ] Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi
    Za dunia ee mwana utuhurumie
  3. [ b ] Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi
    Za dunia ee mwana utujalie amani