Kivumbi

Kivumbi
Performed bySt. Kizito Makuburi
AlbumNyumba ya Roho
CategoryTafakari
ComposerD. Nkoko
Views6,967

Kivumbi Lyrics

  1. Hapo ndipo tulipomfurahia Bwana Mungu wetu
    Hirizi na mizimu yote viliposhindwa kusimama
    Shetani naye kivumbi kakitimua kakimbia

    {Hapo ndipo tukasema hebu Mungu aitwe Mungu
    Hapo ndipo tukasema yeye apewe sifa
    Hapo ndipo tukasema atawale Mungu milele } *2

  2. Tazama Bwana alipounyoosha mkono wake mkuu
    Wachawi wote wakakoma, mapepo na yakanyamaza
    Waganga na tunguri zao kwa aibu wakaduwaa
  3. Bwana alipoinua mkono hodari kwa wagonjwa
    Wakoma wakatakasika viziwi wakasikia
    Viwete wakarukaruka kwa furaha wamepona
  4. Jicho la Bwana lilipowaelekea watu waovu
    Hasira, chuki na majivuno vyote vikatoweka
    Kiburi na maringo yao hapo ndipo vikapotea