Kivumbi
Kivumbi Lyrics
- Hapo ndipo tulipomfurahia Bwana Mungu wetu
Hirizi na mizimu yote viliposhindwa kusimama
Shetani naye kivumbi kakitimua kakimbia
{Hapo ndipo tukasema hebu Mungu aitwe Mungu
Hapo ndipo tukasema yeye apewe sifa
Hapo ndipo tukasema atawale Mungu milele } *2
- Tazama Bwana alipounyoosha mkono wake mkuu
Wachawi wote wakakoma, mapepo na yakanyamaza
Waganga na tunguri zao kwa aibu wakaduwaa
- Bwana alipoinua mkono hodari kwa wagonjwa
Wakoma wakatakasika viziwi wakasikia
Viwete wakarukaruka kwa furaha wamepona
- Jicho la Bwana lilipowaelekea watu waovu
Hasira, chuki na majivuno vyote vikatoweka
Kiburi na maringo yao hapo ndipo vikapotea