Bwana Ninakuita

Bwana Ninakuita
Alt TitleUnifanye Niwe Chombo cha Amani
Performed by-
AlbumIyelele
CategoryInjili na Miito (Gospel)
ComposerVictor Aloyce Murishiwa
Views6,276

Bwana Ninakuita Lyrics

  1. Bwana ninakuita kwa maana utaitika
    Utege sikio lako Mungu wangu
    Bwana usikilize sala nayo maombi yangu
    Unifanye niwe chombo cha amani

    Unifanye niwe chombo cha amani ee Bwana
    Unifanye mimi niwe nuru ya mataifa
    Mashariki magharibi, niende
    Niihubiri imani ya Bwana
    Kaskazini na kusini niende
    Niuhubiri upendo wa Bwana
    { Nitembee pande zote mimi Bwana, ee Bwana
    Nikalitangaze neno lako kwa mataifa } *2

  2. Bwana uniongoze jina lako ni fimbo yangu
    Wewe ndiwe ngao yangu niendapo
    Bwana upendo wako nashindwa kusimulia
    Na ninakupenda sana Mungu wangu
  3. Bwana uniongoze niyashinde majaribu
    Wewe ndiwe ngao yangu niendapo
    Bwana watesi wangu tazama ni wengi sana
    Niongoze nimshinde mwovu shetani