Uko Juu

Uko Juu
Performed by-
CategoryTafakari
ComposerBernard Mukasa
Views6,253

Uko Juu Lyrics

  1. Hufanani nasi, unang'ara na tena una enzi, una utukufu
    Umepita zote, sifa tunazokutolea sisi, nao malaika oho

    Wewe uko juu umetukuka na tunakuinua kwa nyimbo zetu hizi

  2. Walikuimbia, baba zetu lakini hazikwisha, sifa zako wewe
    Na watakatifu, wanaimba na hazimaliziki, tenzi hazitoshi oho
  3. Mimea ya nchi, yaeleza inapopukutika, kuhifadhi maji
    Kwamba wewe Bwana, hupungui unajua kuumba, hupitiwi neno oho
  4. Kinyonga mdogo, anageuka rangi kujilinda, bila ya bunduki.
    Anafafanua, umakini ndani ya kazi yako, isiyo dosari oho
  5. Na uhimidiwe, wewe Baba yaani ndiwe Mwana, Roho Mtukufu,
    Ulivyotukuzwa, enzi zile sasa hata milele, utukuzwe pote oho