Uko Juu
   
    
     
        | Uko Juu | 
|---|
| Performed by | - | 
| Category | Tafakari | 
| Composer | Bernard Mukasa | 
| Views | 6,549 | 
Uko Juu Lyrics
 
             
            
- Hufanani nasi, unang'ara na tena una enzi, una utukufu
 Umepita zote, sifa tunazokutolea sisi, nao malaika oho
 Wewe uko juu umetukuka na tunakuinua kwa nyimbo zetu hizi
- Walikuimbia, baba zetu lakini hazikwisha, sifa zako wewe
 Na watakatifu, wanaimba na hazimaliziki, tenzi hazitoshi oho
- Mimea ya nchi, yaeleza inapopukutika, kuhifadhi maji
 Kwamba wewe Bwana, hupungui unajua kuumba, hupitiwi neno oho
- Kinyonga mdogo, anageuka rangi kujilinda, bila ya bunduki.
 Anafafanua, umakini ndani ya kazi yako, isiyo dosari oho
- Na uhimidiwe, wewe Baba yaani ndiwe Mwana, Roho Mtukufu,
 Ulivyotukuzwa, enzi zile sasa hata milele, utukuzwe pote oho