Mlipuko wa Sifa

Mlipuko wa Sifa
Performed bySt. Yuda Thadei Mbeya
AlbumMlipuko wa Sifa
CategoryEntrance / Mwanzo
ComposerBernard Mukasa
Views17,060

Mlipuko wa Sifa Lyrics

  1. [ s ] Zikumbukeni njia alizowapitisha
    [ w ] Amewapenda amewang`ang`ania ninyi
    Hajaufumba ukope wake hata mara moja
    Amewapenda amewang`ang`ania ninyi
    Hajazifumbua mbawa zake msilowe mvua
    Amewapenda amewang`ang`ania ah

    Lipua pu! pu! pu pu pu! puu!
    Lipua sifa - sifa kwa Mungu Baba lipua
    Lipua shangwe- sifa kwa Mungu Baba lipua
    Lipua tena - sifa kwa Mungu Baba lipua aa
    (amsheni hisia, lipua sifa, inueni mioyo lipua sifa)
    Lipua lipua lipua aa lipua lipua, lipua puu

  2. Kumbuka mlivyokuwa na hali duni kule mwanzo,
    Ni yeye Mungu aliyewabeba
    Mlipopotea njia akawakamata mkono . . .
    Ni yeye Mungu aliyewabeba
    Akawaongoza mpaka kufika mlipo leo . . .
    Ni yeye Mungu aliyewabeba
  3. [ b ] Kusanyikeni wote kwa miluzi na nyimbo tumtukuze,
    Paza sauti zenu piga kelele kumsifu
    Cheza kidogo wote inueni mikono shangilieni.
    Paza sauti zenu piga kelele kumsifu
    Rusha miguu yenu kwa midundo mitamu tumtukuze . . .
    Paza sauti zenu piga kelele kumsifu

    Paza sauti - zenu piga kelele kumsifu
    Nyinyi na nyumba - zenu piga kelele kumsifu
    Na majirani -zenu piga kelele eh
    ~ ~ ~
    Tunampigia aah ngoma tamu
    Tunamchezea aah ngoma tamu kabisa
    Tumpigie - vigelegele makofi *6