Mimi Nimeumbika

Mimi Nimeumbika
Performed bySt. Don Bosco Kyaani
AlbumWashuhuda wa Yesu
CategoryThanksgiving / Shukrani
ComposerEmmanuel Kawa
Views3,386

Mimi Nimeumbika Lyrics

  1. { Mimi oh! oh oh! mimi oh! oh oh!
    Niumbika mimi kweli napendeza } *2
    { Nitakuimbia, nitakuchezea
    Asante Baba kuniumba jinsi nilivyo } *2

  2. Nampenda Bwana kwa kuwa ananisikiliza
    Huisikiliza sauti yangu na dua zangu
    Hunitegea sikio lake nimwitapo yeye
    Kwa hivyo nitaliita jina lake siku zote
  3. Kamba za mauti ziliponizunguka mimi
    Shida za kuzimu zikaniandama sana
    Niliona tabu nyingi nikamlilia Bwana wangu
    Nami nikaliita jina lake akaniokoa
  4. Bwana katujalia sauti nzuri ya kupendeza
    Ili tumwimbie yeye siku zote maishani
    Kwa hivyo yatupasa sote kumwimbia yeye
    Kwani Mungu wetu ni mkarimu kwa watu wote