Mimi Nimeumbika
Mimi Nimeumbika Lyrics
{ Mimi oh! oh oh! mimi oh! oh oh!
Niumbika mimi kweli napendeza } *2
{ Nitakuimbia, nitakuchezea
Asante Baba kuniumba jinsi nilivyo } *2
- Nampenda Bwana kwa kuwa ananisikiliza
Huisikiliza sauti yangu na dua zangu
Hunitegea sikio lake nimwitapo yeye
Kwa hivyo nitaliita jina lake siku zote
- Kamba za mauti ziliponizunguka mimi
Shida za kuzimu zikaniandama sana
Niliona tabu nyingi nikamlilia Bwana wangu
Nami nikaliita jina lake akaniokoa
- Bwana katujalia sauti nzuri ya kupendeza
Ili tumwimbie yeye siku zote maishani
Kwa hivyo yatupasa sote kumwimbia yeye
Kwani Mungu wetu ni mkarimu kwa watu wote