Wangu wa Milele

Wangu wa Milele
Performed by-
CategoryHarusi
ComposerS. Ndibalema
Views7,053

Wangu wa Milele Lyrics

  1. Mpenzi wangu ungana nami, tumshukuru Mungu wetu
    Uje tucheze kwa furaha, tumshukuru Mungu wetu
    Kwani ile siku tuliyoingojea - iwe tumshukuru Mungu wetu
    Mwenyezi ametujalia - iwe, tumshukuru Mungu wetu

  2. Nasema mbele ya wazazi wako (ni wewe)
    Ni wewe niliyekuchagua (ni wewe)
    Nasema mbele ya wazazi wangu, ni we wangu wa moyoni
    Ninatamka mbele za Mungu (ni wewe)
    Mtima wangu nakupatia (ni wewe)
    Nasema mbele ya wazazi wangu, Ni we wo mtima gwange
  3. Unawaacha wazazi wako (ni wewe)
    Mwili mmoja tunakuwa (ni wewe)
    Nami nitakupenda milele, Ni we wangu wa moyoni
    Ninawaacha wazazi wangu (ni wewe)
    Mwili mmoja tunakuwa (ni wewe)
    Nami nitakupenda milele, Ni we wo mtima gwange
  4. Ndi-we mama wa watoto wangu (ni wewe)
    Mwenyezi Mungu kanipatia (ni wewe)
    Karibu kwetu kipenzi changu, ni we wangu wa moyoni
    Ndi-we baba wa watoto wangu (ni wewe)
    Mwenyezi Mungu kanipatia (ni wewe)
    Nakuja kwenu kipenzi changu, Ni we wo mtima gwange
  5. Nawashukuru wazazi wako, umbo zuri wameniletea
    Namshukuru Mwenyezi Mungu, ni we wangu wa moyoni
    Nawashukuru wazazi wako, lulu yangu walinitunzia
    Haki ya Mungu nitakutunza, ni we wo mtima gwange
Kihaya Melody